Bado nina mipango na Fabregas - Antonio Conte

Kocha wa Chelsea Antonio Conte, amesema kiungo Cesc Fabregas bado ana mipango naye licha ya kutompanga kwenye mchezo wa jana wa ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya West Ham, katika uwanja wa Stamford Bridge.
Cesc Fabregas
Bao la Costa, kunako dakika ya 89, liliihakikishia Chelsea pointi 3 muhimu, baada ya James Collins, kusawazishia West Ham, wakati Eden Hazard alikuwa ameshaandika bao la kwanza kwa The Blues kwa njia ya peanati.
"Inaweza kutokea kwa mchezaji yoyote kumwacha kwenye kikosi cha kwanza, kama nilivyomwacha Fabregas, muhimu kuona hilo ni jambo jema, kwa sababu ni lazima tupigane kwenye msimu huu, na muhimu kukaa pamoja kwa kila hali".Alisema Conte.
Fabregas aliyeachwa kwenye benchi, amekuwa akihusishwa na kutaka kutimka kwenye klabu hiyo ya darajani ambapo inasemakana huenda akakimbilia vilabu vya Real Madrid, Juventus au klabu yake ya zamani, Barcelona

0 maoni:

Chapisha Maoni

RAIS DKT. MAGUFULI AWAJULIA HALI SPIKA WA BUNGE JOB NDUGAI PAMOJA NA WAZIRI MKUU MSTAAFU JOHN SAMUEL MALECELA JIJINI DAR ES SALAAM

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana kwa furaha na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili nyumbani kwake Sala sala nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai nyumbani kwake Sala sala jijini Dar es Salaam alipokwenda kumjulia hali.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli kushoto akizungumza jambo na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai nyumbani kwake Sala sala jijini Dar es Salaam walipokwenda kumjulia hali. Kulia ni mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akisalimiana na  Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwasili nyumbani kwa Spika Sala sala jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimjulia hali Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela ambaye anapata matibabu jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akimsalimia Waziri Mkuu mstaafu John Samuel Malecela ambaye anapata matibabu jijini Dar es Salaam.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwa pamoja na Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiongoza Sala ya kumuombea Waziri Mkuu mstaafu John Samwel Malecela pamoja na mkewe Anne Kilango Malecela.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akizungumza na Mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai wakati alipokwenda na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwajulia hali nyumbani kwao Sala sala jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na mke wa Spika Dkt. Fatma Mganga Ndugai huku Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiagana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Job Ndugai mara baada ya kuwajulia hali nyumbani kwao Sala sala jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU







0 maoni:

Chapisha Maoni

KUNDI LA ORIGINAL COMEDY LAINGIA MATATANI KWA KUVAA SARE ZA POLISI KWENYE HARUSI YA MASANJA MKANDAMIZAJI

Katika siku za hivi karibuni, kumejitokeza  tabia kwa baadhi ya watu wakiwemo wasanii watu wengine mmoja mmoja kutumia mavazi yanayofanana na sare za Majeshi ya Ulinzi na usalama hapa nchini likiwemo Jeshi la Polisi katika shughuli zao za kisanii au katika kazi mbalimbali, Jambo ambalo ni kinyume cha sheria, kanuni na taratibu za Nchi.


Kwa mujibu wa Sheria ya kanuni za makosa ya Jinai, sura ya 16 na  marejeo yake ya mwaka 2002,  kifungu cha 178 (1) na  (2) kinachozungumzia makosa dhidi ya sare za majeshi ya ulinzi na usalama,  kinabainisha wazi kuwa ni kosa kisheria kwa mtu yeyote ambaye siyo mtumishi wa majeshi ya ulinzi na usalama kuvaa mavazi yanayotumiwa au kushabihiana na sare za majeshi hayo  bila kibali kutoka kwa  Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kufuatia  kitendo kilichofanywa na kundi la kisanii la “ Original Comedy” kuvaa mavazi yanayoshabihiana na sare za Jeshi la Polisi, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar Es Salaam linachukua  hatua za kisheria dhidi ya wasanii hao.
Aidha Jeshi la Polisi nchini, linatoa onyo kali kwa mtu ama kikundi chochote kuacha kutumia  mavazi yanayofanana na sare zinazovaliwa na  majeshi ya ulinzi na usalama hapa nchini na atakayebainika hatutasita kuchukua hatua kali za kisheria dhidi yake.
Jeshi la Polisi linatoa rai kwa wale wote wenye mavazi yanayoshabihiana na sare za majeshi ya ulinzi na usalama  kuzisalimisha mara moja katika vituo vya Polisi vilivyokaribu nao.
 Imetolewa na:
Advera John  Bulimba – Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP)
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
                                                        Makao Makuu ya Polisi.     

0 maoni:

Chapisha Maoni

Google wamezindua program mpya na itakuwa ni bure kwa watumiaji wa simu

Kampuni ya Google imezindua programu yake mpya kwa jina DUO. Programu hiyo ni jibu la Google kwa programu nyengine kama ile ya Apple ya Face Time,Skype ya Microsoft na Facebook messanger.


Programu hii haina tofauti kubwa na programu nyingine zinazotoa huduma za video, isipokuwa inakupatia uwezo wa ni nani anayepiga simu hivyo basi kumpatia mtumiaji fursa ya kuamua iwapo ataipokea simu hiyo au la. Programu hiyo mpya iliotangazwa mwezi May imezinduliwa kama huduma ya bure kwa simu zinazotumia Android pamoja na simu za Apple za iPhone.
Simu zinalindwa na haziwezi kudukuliwa na video hubadilika kulingana na kasi ya kushika simu inayopigwa. Kama programu ya FaceTime, duo inahitaji nambari ya mtu ya simu kuunganishwa. Huduma nyingine zinahitaji mtumiaji kuingia katika akaunti zao ili kupata fursa ya kupata huduma hiyo.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Yannick Bolasie adondosha wino Everton kutokea Crystal Palace

Klabu ya Everton imetangaza kumsajili kiungo Yannick Bolasie kutokea Crystal Palace kwa ada ya pauni milioni 25.
Mchezaji huyo kwa kimataifa wa DR Congo,27, amesaini mkataba wa miaka mitano kunako klabu hiyo.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Obama kukamilisha ahadi ya kulifunga gereza la Guantanamo Bay

Marekani imetangaza kuwahamisha wafungwa 15 waliokuwa kwenye gereza la Guantanamo Bay nchini Cuba na kupelekwa Emirates.
Taarifa ya kuhamishwa kwa wafungwa hao imetolewa kutoka makao makuu ya jeshi la nchi hiyo lililopo Pentagon na kati ya wafungwa hao 12 wanatoka Yemen na watatu Afghanistan.
Kundi la watu hao ni moja kati ya kundi kubwa la wafungwa kuwahi kuhamishwa kutoka kwenye gereza hilo chini ya utawala wa Rais Barack Obama tangu mwaka 2008. Mpaka sasa idadi ya wafungwa waliobakia kwenye gereza hilo imefikia 61 hatua ambayo imeonekana kupingwa vikali na Chama cha Republican chini ya mgombea wake Donald Trump.
Hata hivyo mara kadhaa Rais Obama ameeleza masikitiko yake juu ya msimamo wa chama hicho wa kupinga mpango wake wa kutaka kufunga gereza hilo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi yake aliyowahi kuitoa wakati wa kampeni za Urais.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Mambo manne yaliyoafikiwa kwenye kikao cha dharura kuhusu kusudio la Manji kujitoa Yanga

August 16 2016 ikiwa ni siku moja imepita toka kuenea kwa habari katika mitandao ya kijamii kuwa mwenyekiti wa Yanga Yusuph Manji amejiuzulu nafasi yake ya uenyekiti kwa madai ya kuandamwa na maneno na kujihisi mpweke kwani hakuna mwanachama yoyote wa Yanga aliyeonesha kuwa upande wake.
Baada ya taarifa hizo kuenea viongozi wa kanda wa Yanga walikaa na kuamua kufanya mkutano wa dharura leo August 16 makao makuu ya klabu yao,  moja kati ya viongozi wa matawi ya Yanga mkoa wa Dar es Salaam anayeiwakilisha kanda ya Temeke Robert Liungu ametaja maazimio waliyofikia kutoka katika mkutano wa dharura.
1- Wanachama wa Yanga wanatambua kuwa Manji bado ni mwenyekiti wao kwa mujibu wa katiba yao.
2- Wanachama wamemuomba mdhamini Mzee Katunda amtoe mzee Akilimali anayedaiwa kumpinga Manji atolewe katika nafasi ya katibu wa wazee wa Yanga.
3- Wanachama wanaiomba kamati ya utendaji ya Yanga imuite mzee Akilimali imuhoji na kumsimamisha uanachama kwa madai kuwa yeye ni Simba. 
4- Wanachama wa matawi yote wanaendelea kumtambua Yusuph Manji kama mwenyekiti wao

0 maoni:

Chapisha Maoni

Dully Sykes adai awali alipanga kumshirikisha Diamond kwenye Inde

Dully Sykes amedai kuwa awali alipanga kumshirikisha Diamond kwenye wimbo wake Inde aliofanya na msanii wa WCB, Harmonize.
Akiongea na kipindi cha 180 Power cha Sibuka FM, Dully alisema baada ya kuona Diamond yupo busy, kura yake ilimwangukia Harmonize.
“Huu wimbo kwanza nilipenda kufanya na Diamond,” alisema muimbaji huyo mkongwe.
“Lakini nikaona Diamond yuko busy sana nisimsumbue, nikaangalia after Diamond nani anastahili, nikaona Harmonize anafaa kati ya vijana niliowafikiria.”
Inde umekuwa wimbo wenye mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi huku video yake ikiwa na zaidi ya views 480k hadi sasa.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Ni muda wa kuisubiri P-Square mpya

Hatimaye maombi na dua za mashabiki wa kundi la P-Square yamekamilika baada ya ujumbe wa Paul Okoye kuonyesha kurudi upya kwa kundi hilo.
Ni muda mrefu umepita tangu kundi hilo linaloundwa na ndugu wawili ambao ni Peter na Paul Okoye kuvunjika na kila mmoja kufanya kazi kivyake. Wakati wa kuvunjika kundi hilo Peter aliachia wimbo wake wa kwanza akiwa mwenyewe ‘Kiss Kiss’ na ‘Look Into My Eyes’ huku akitumia jina la Mr P na Paul alianza kutumia jina la Rude Boy huku akifungua lebo yake iliyokuwa ikiwasimamia wasanii wawili.
Hakika baada ya hatua hiyo muziki wa Nigeria ulionekana kukosa ladha kama tomato unapoikosa kwenye kiepe japo haishibishi hata ukiikosa lakini utatamani kukirudisha kwa muuzaji.
Paul alionekana mara kadhaa kuchukizwa kuvunjika kwa kundi hilo huku akimuomba ndugu yake warudi wafanye kazi kwa pamoja kama zamani lakini kwa wakati huo ilishindikana. “Mpendwa kaka yangu nakuomba, hata kama humtaki tena Jude na hauitaki P-Square, milele utakuwa kaka yangu. Lakini natamani sisi watatu tungeendelea kuwa pamoja sababu ni kitu cha furaha,” aliwahi kuandika Paul Okoye kwenye mtandao wake wa Instagram.
“Watu wanatupenda sana si sababu tu ya muziki wetu mzuri, lakini kuwaona ndugu wakiwa pamoja, kuwa mfano mzuri kwa familia zingine na kwa watoto wetu. Tafadhali, jishushe, samehe na sahau, bado tunaweza kubadilisha hili jambo. Kama nilisema chochote au kufanya chochote nilichokuumiza, nisamehe. Na kwa mashabiki wetu wote wa ukweli, tafadhali tuombeeni. Mungu awabariki wote.”
Hata hivyo mara kadhaa Peter ameonekana kukaa kimya bila kuzungumza chochote huku akiendelea kufanya show peke yake kwa kuzunguka nchi kadhaa ikiwemo Dubai na nchi zingine.
Wimbo wa ‘Kidogo’ wa Diamond ndiyo ulikuwa wimbo wa kwanza wasanii hao ndugu kuonekana mara ya kwanza kwenye video wakiwa pamoja tangu lilipovunjika kundi lao na kuwafanya mashabiki waliowazoea kufurahia kitendo hicho huku wakiwa na matumaini mapya ya kurudi tena kwa kundi hilo.
Mwezi Julai mwaka huu hatimaye aliyekuwa mgumu wa kubadili maamuzi yake, Peter alipost kipande cha video akiahidi kurudi tena na kuwaomba radhi mashabiki wao kwa yaliyotokea lakini pia alitangaza kumrejesha kaka yao, Jude Okoye kama meneja wao. “Something new Cooking in da kitchen and about to come out! From us! You already know it’s P2 baby!!! #KoolestDudes,” aliandika Peter kwenye post yake aliyoiweka kwenye instagram hivi karibuni.
Picha mpya ya Peter na Paul Okoye waliyopiga hivi karibuni
Hatimaye Paul Okoye ameonekana kufurahia uamuzi huo wa ndugu yake na ameonekana kumsamehe ndugu yake kwa moyo mmoja baada ya hivi karibuni kuweka picha mbili kwenye mtandao wake wa Instagram alizopiga na ndugu yake huyo na kuandika, “History 😎 it’s all Good 😎.” “Family is everything 😎👍,” aliandika kwenye picha nyingine.
Penye nia pana njia, hakika maombi ya mashabiki hao yanaonekana yameanza kukamilika ni muda wa kusubiri chakula wanachotuandalia huko jikoni.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Makonda akabidhi ramani ya ofisi mpya za Bakwata

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amekabidhi ramani ya jengo la kisasa la ghorofa tatu litakalokuwa ofisi ya Mufti wa BAKWATA nchini litakalojengwa kupitia wafadhili mbalimbali na litagharimu shilingi bilioni 5.08.
Amekabidhi ramani hiyo Jumatatu hii katika hafla iliyofanyika baada ya sala ya adhuhuri katika viwanja vya BAKWATA Kinondoni jijini Dar es salaam.
“Leo nimefika hapa ikiwa ni mwanzo wa safari mpya ya serikali ya mkoa wa Dar kujenga makao makuu mpya ya kisasa ya ndugu zangu, viongozi wangu wa BAKWATA, najua watu wote wana viongozi kama baba ni kiongozi wa familia, watu wana vyama vyao vya siasa wana viongozi,watu wana makampuni yao wana viongozi lakini viongozi hawa wanatofautiana na viongozi wa dini kwa jambo moja, viongozi wa dini wanatuongoza kutupeleka kwa mola alietuumba sote”, alisema Makonda
Kwa upande wake Mufti mkuu wa Dar es Salaam, Abubakar Zubeir alisema, “kila mwenye uwezo wa kuweza kusaidia jambo hili basi anyooshe mkono kusaidia, hakuna jambo ambalo linafaa kusaidia kama mambo ya heri na ya Kimungu, ukisaidia jambo la kimungu umesaidia Mungu apatikane pale, watu kumtaja Mungu pale, umesaidia watu kumjua Mungu, utakuwa umesaidia watu kujifunza maadili mema na pia utasaidia mambo ya kulinda amani na kutunza nchi,” alisema Mufti huyo.
Naye Sheikh mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum alisema, “leo tunashuhudia Makonda anakuja kufanya kitu ndani ya makao makuu ya BAKWATA hizi harakati zinatokana na wazazi wako wako waliokulea inaonyesha baraka kubwa,vitu hivi vinakuwa vya baraka.”
Makonda alimaliza kwa kusema viongozi wa dini wana mchango mkubwa katika kuhamasisha amani na kulinda amani. Mwishoni masheikh walikuwa na dua maalum ya kumuombea mkuu huyo wa mkoa.
BY: EMMY MWAIPOPO

0 maoni:

Chapisha Maoni

Wema aelezea bidhaa yake mpya na alikopata wazo la biashara hiyo

Nguvu ya mwigizaji staa wa Tanzania Wema Sepetu  kutengeneza zaidi bidhaa zenye jina lake na kuziuza kwa Watanzania inaendelea kuonekana, ni juzijuzi tu alileta lipstick zenye jina la KISS BY WEMA.
wema kuyaongea haya>>>Mimi naweza kusema kwamba idea imetoka kwa Mama  kwamba anapenda sana vitu vya asili ukienda nyumba kwa Mama yangu utakuta viatu vyake vingi vya kimasai na hii ni idea yake’

‘Baada ya hapo tukaanza kutafuta Jinsi ya kutengeneza za kwetu mwisho wa siku tukapata sample nzuri kwahiyo ni kitu ambacho nimemfanyia Mama yangu’- Wema

0 maoni:

Chapisha Maoni

Nimeshakuwa sasa, kiukweli nina kiu ya mume – Johari

Msanii wa filamu, Johari Chagula amefunguka kwa kusema kuwa kwa sasa ana kiu yakumpata mume sahihi ambaye ataingia naye kwenye maisha ya ndoa.
Mwigizaji huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja, amesema umri wake kwa sasa unamruhusu kuingia kwenye maisha ya ndoa
“Mimi ni mwanamke kamili, ni mtu mzima. Nimeshakuwa sasa, kwahiyo kiukweli nina kiu ya mume,” Johari aliliambia gazeti la Mtanzania. “Mungu akinipa mume bora, nitaolewa. Sitaki kuzungumzia sana mambo yaliyopita, lakini muhimu kwa sasa ni mume,”
Mbali na hayo mwingizaji huyo amewataka kukaa mkao wa kula kwa ajili ya filamu yake mpya ambayo amewashirikisha wasanii wachanga kutoka mkoani Mwanza.

0 maoni:

Chapisha Maoni

je ni kweli Mwimbaji Emmanuel Mbasha karudiana na Flora Mbasha majibu haya hapa.......

Kama utakuwa unakumbuka mnamo September 21,2015 moja ya stori kubwa iliyogusa kwenye kurasa za Magazeti ya Tanzania ni ishu ya Hukumu ya Kesi ya Mwimbaji wa Gospel Tanzania, Emmanuel Mbasha ambapo alikuwa anakabiliwa na Keshi ya kumbaka shemeji yake na kesi imekuwa Mahakamani tangu 2014.
wengi tunafahamu kwamba mwimbaji huyo aliachiwa huru baada ya Mahakama kumkuta hana hatia kwenye Kesi hiyo, sasa leo kajibu swali kuhusu kurudiana na mkewe Flora Mbasha na kuyaongea haya>>

‘Mimi kurudiana na Flora Mbasha ni ngumu kwasababu yeye ndio aliniacha mimi na yeye ndio aliandaa mazingira yake ya kuniacha mimi mpaka ikafika wakati Familia yangu, viongozi mbalimbali wa Dini wakawa wanamshauri lakini akutaka kurudiana na mimi kwahiyo naweza sema ni ngumu kurudiana na Flora’

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kimetajwa hapa kiasi cha Pesa alichokuwa akilipwa Hanscana na Wanene Entertainment.

Kama ulikuwa una shauku ya kujua kiasi cha pesa ambacho muongozaji wa video nchini Hanscana alikuwa analipwa na studio za Wanene,uongozi wa studio hizo wametaja kiasi walichokuwa wakimlipa director Hanscana.
Akiongea kwenye kipindi cha funiko base,Gentriez ambaye ni mmoja watu wa ndani wa kampuni hiyo amesema Hascana alikuwa analipwa sjilingi milioni mbili kila mwezi na studio hizo na pia video zote alizokuwa akizifanya pesa zilikuwa zinaingia kwa Hanscana.
Wanene tulikuwa tunamlipa mshahara hata kabla kampuni haijafunguliwa tulikuwa tunamlipa na video alizokuwa akifanya pesa yote ilikuwa inaingia mfuko kwa Hascana kwa hiyo wanene walikuwa wamewekeza kwake lakini baada ya kufungua kampuni ilibidi kwenye kila kazi lazima kuwe na percent ya kampuni..tulikuwa tunamlipa milioni mbili kwa mwezi” alifunguka Gentriez

0 maoni:

Chapisha Maoni

Too Much ndio video iliyomtesa zaidi Darassa,mwenyewe amefunguka hapa..

Msanii wa rap Tanzania,Darassa amefunguka na kusema kuwa video yake ya wimbo wa Too Much ndio video ambayo imemtesa zaidi kwenye kuifanya.
Akiongea kwenye kipindi cha funiko Base cha radio 5,Darassa amesema imemgharimu muda mwingi na pesa nyingi kuikamilisha video hiyo kwani alitaka kufanya kitu kikibwa kwenye uwanja wa nyumbani.
Too Much kwangu ni video kubwa na imetu cost,imetuchukua muda,imetuumiza hapa ninavyoongea hakuna tulichobakiwa nacho zaidi ya nguvu na akili tu.Tulichokuwa tunataka ni kuhakikisha tunatengeneza video nzuri nyumbani hata tukifanikiwa kimataifa watu wajue jamaa ameendelea tu ila alianzia nyumbani ndio tunachopambania,watu wa nje wahitaji kufanya kazi na sisi” alifunguka Darassa.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Nay wa Mitego adai Mr Ttouch anamchukulia kama mtoto aliyefikia umri wa kuondoka nyumbani

Rapper Nay wa Mitego amefunguka na kuzungumza madai ya kugombana na kuachana na mtayarishaji wake mahiri wa studio yake ya Free Nation, Mr Ttouch.
Wawili hao kwa sasa kila mmoja anafanya kazi kivyake baada ya kudaiwa kuhitilafiana kwenye masuwala ya pesa.
Akiongea na Bongo5 Jumatatu hii, Nay wa Mitego amesema yeye hajagombana na Mr Ttouch kama baadhi ya watu wanavyosema.
“Mimi kwangu namchukulia Mr T kama mtoto aliyekuwa nyumbani na sasa amekuwa mtu mzima anaamua kutafuta maisha yake, kwa hiyo mimi namtakia mafanikio mema katika maisha yake,” alisema Nay.
“Mimi ndiye niliyemtafuta Mr T na kuamua kumkabidhi studio, nikawa sichukui hata shilingi mia, kwa hiyo mimi nachoweza kusema muache aende kwa sababu amekuwa mtu mzima,” aliongeza.
Pia rapper huyo amesema kwa sasa kama ana kazi atamtafuta mtayarishi huyo kwa ajili ya kazi lakini hawezi tena kufanya naye kazi kishkaji kama zamani.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Wanene Entertainment waweka wazi sababu za Hanscana kujitoa kwenye kampuni hiyo..

Baada ya muongozaji wa video nchini Hanscana kujitoa kwenye kampuni iliyokuwa ikimsamimia,Wanene Entertainment,kwa upande wao (Wanene) wamefunguka na kusema kuwa hakuna ugomvi kati yao na Hanscana bali tu walishindwa kukubaliana kwenye vitu kadhaa.
Akiongea kwenye mahojiano na radio 5,Gentriez ambaye ni mmoja kati ya watu wa ndani wa kampuni hiyo amesema kuwa Hanscanah alisema anataka atimiziwe vitu kadhaa la sivyo angevunja mkataba na ndichi kilichotokea.
Ni kweli Hanscana hayupo wanene Entertainment,hajafukuzwa lakini amejiuzulu kutokana na mkataba aliopewa na kampuni hakuwa ameuridhia.Yeye alitaka mahitaji fulani kwa kampuni kama Red camera,ili afanye kazi kwa ufanisi zaidi,lakini kampuni ilimwambia asubiri kidogo atumie zilizopo halafu mbeleni atapata hiyo camera maana ni hela ndefu kidogo,pia alikuwa analalamika kuwa kampuni imewekeza hela nyingi kwenye audio kuliko video,n hivyo tu hakuna bifu yoyote” alieleza Gentriez

0 maoni:

Chapisha Maoni

Harmonize: Nivae dela ndio mseme simkopi Diamond?

Shutuma kuwa amekuwa akimuiga bosi wake Diamond, zimemchosha Harmonize na sasa ameamua kujibu.
Baada ya video ya wimbo Inde alioshirikishwa na Dully Sykes kutoka, mashabiki ndio wamezidi kuendelea kusisitiza kuwa msanii huyo anamuiga kwa kiasi kikubwa Diamond.
Harmonize ambaye mara nyingi amekuwa akisisitiza kuwa ndivyo yeye alivyo na yeye sasa ameonekana kuchoshwa na malalamiko ya mashabiki hao ambapo amejikuta akiandika ujumbe wenye utata kwenye Instagram:

0 maoni:

Chapisha Maoni

Kisa kusakamwa na Mashabiki: Justin Bieber aifuta akaunti yake ya Instagram



Justin Bieber alitishia kuiweka akaunti yake ya Instagram private kama mashabiki wake hawataacha kumshambulia mpenzi wake, Sofia Richie.
Lakini staa huyo alichukua hatua kubwa zaidi kwa kuifuta akaunti yake ya Instagram yenye followers, milioni 77.8. Awali alianza kwa kuiweka private na kubadilisha mawazo yake kuirudisha kawaida tena kabla ya kuifuta kabisa.
. 
Staa huyo mwanzoni aliandika:
‘I’m gonna make my Instagram private if you guys don’t stop the hate this is getting out of hand, if you guys are really fans you wouldn’t be so mean to people that I like.’
Lakini kutoka kusikojulikanam ex wake, Selena Gomez alimshambulia kwa kuandika: If you can’t handle the hate then stop posting pictures of your girlfriend lol – it should be special between you two only. Don’t be mad at your fans. They love you.’
Mambo yalibadilika na JB kujibu: ‘It’s funny to see people that used me for attention and still trying to point the finger this way. Sad. All love. I’m not one for anyone receiving hate.’
Ujumbe wa Bieber ulimchokonoa zaidi Gomez aliyejibu: Funny how the ones that cheated multiple times, are pointing the finger at the ones that were forgiving and supportive, no wonder fans are mad. Sad. All love.’
Bieber hakukaa kimya, alijibu: I cheated… Oh I forgot about You and Zayn?’

0 maoni:

Chapisha Maoni

KESSEBOY WA KIGOLI KAAMUA KUOKOA NA KUJIITA KESSE NJONJOO


0 maoni:

Chapisha Maoni

Uchaguzi Zambia: Rais Edgar Lungu aibuka mshindi

Rais wa Zambia Edgar Lungu ametangazwa mshindi matokeo ya uchaguzi wa urais kulingana na matokeo rasmi ya uchaguzi huo.
August 15 2016 Tume ya uchaguzi nchini Zambia ilimtangaza aliyekuwa rais wa Zambia, Edgar Lungu kuwa ndo mshindi wa nafasi hiyo ya urais kwa tiketi ya chama cha Patriotic Front kwa awamu ya pili. Lungu alipata asilimia 50.35 ambazo ni sawa na kura 1, 860, 877 na Kumshinda mpinzani wake Hakande Hichilema wa chama cha United Party for National Development ambaye amepata asilimia 47.67 ambazo ni kura 1, 760, 347.
Matokeo hayo yametangazwa Jumatatu hii japo mpinzani wake, Hakainde Hichilema akidai kuna udanganyifu katika uhesabuji wa kura. Matokeo hayo yamempa ushindi Rais Lungu kwa zaidi ya kura laki moja mbele ya mpinzani wake huyo wa karibu.
Siku ya Jumapili, Hichilema akiongozana na wafuasi wake, walifika kwenye makao makuu ya tume ya uchaguzi ya Zambia ambako matokeo yanatangaziwa akitaka kukutana na mwenyekiti wa tume, lakini hata hivyo alizuiliwa na Polisi.
Hichilema wa UPND ameyapingwa matokeo hayo.
Anadai kulikuwa na udanganyifu mkubwa wa kura kwenye jimbo la Lusaka na maeneo mengine ya nchi, ambako anasema tume ya uchaguzi ilichelewa kutangaza matokeo yake kwakuwa yalikuwa yakitengenezwa ili kumpa ushindi Rais Lungu ambaye anatetea kwa mara nyingine nafasi yake.
Uchaguzi wa mwaka huu ulikuwa wa upinzani mkali kati ya Rais Lungu, ambaye pia alimshinda Hichilema kwenye uchaguzi uliopita kwa kura elfu 28, na safari hii mchuano ulikuwa mkali zaidi kutokana na upinzani ulioshuhudiwa.
Hata hivyo wadadisi wa mambo wanaamini kuwa uchaguzi wenyewe ulikuwa na mapungufu, ikiwemo vitisho kwa baadhi ya maofisa wa tume, lakini kwa sehemu kubwa wanakubaliana kuwa ulifanyika kwa huru na haki.
Waangalizi wengi wa kimataifa kwenye ripoti zao za awali waliwapongeza wananchi wa Zambia kwa kushiriki uchaguzi kwa amani licha ya dosari ndogondogo ambazo walizibaini ingawa hawajasema ikiwa uchaguzi ulikuwa wakuaminika.
Wakati akihitimisha kampeni zake Rais Lungu aliahidi kuilinda katiba ya nchi kwa kuhakikisha usalama wa raia dhidi ya watu waliodaiwa kutaka kufanya vurugu.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Picha,Tyga katoa hili gari kama zawadi kwenye birthday ya mpenzi wake Kylie Jenner.

Mpenzi wa rapa Tyga amepokea zawadi nyingine ya kifahari kutoka kwa mpenzi wake. Rapa Tyga amempa Kylie Jenner gari mpya aina ya Maybach kwenye siku yake ya kuzaliwa akiwa anafikisha miaka 19.
Tyga aliwasiliana na kampuni inayotoa magari kwa watu maarufu ya Richie Rich, na gari hio imelipiwa dola laki mbili na mbili na elfu ishirini.
Kylie anafikisha miaka 19 mnamo August 10.
Mwaka jana Tyga alimpa gari mpenzi wake huyu alipofikisha miaka 18, ilikuwa ni gari aina ya Ferrari 458 convertible.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Watoto wamiminika katika kambi ya tiba ya vichwa vikubwa na mgongo wazi Songea

Zaidi ya watoto 50 Jumapili hii wamehudhuria kambi tiba ya GSM Foundation inayoendeshwa kwa ushirikiano na Taasisi ya Mifupa na upasuaji ya MOI, yenye lengo la kupunguza vifo na mtindio wa ubongo kwa watoto wanaozaliwa na vichwa vikubwa na mgongo wazi, ambayo leo imeingia katika mkoa wa pili katika msimu wake wa pili pia, wenye lengo la kuwafanyia upasuaji watoto 100.
Wagonjwa wakisajiliwa katika chumba maalum cha kuwapokea katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma

Kaimu Mkuu wa kambi hiyo iliyoanzia mkoani Mtwara Jumanne ya tarehe 2 mwezi huu, DK Shaaban Hamis, amesema, muitikio walioupata katika mkoa huu ni muitikio mkubwa zaidi ukilinganisha na mkoa wa Mtwara, ambako ndio kunakosadikika kuwa na wagonjwa wengi zaidi, kutokana na rekodi waliyonayo, baada ya tafiti mbali mbali.
“Inawezekana hapa tukafanyia upasuaji wagonjwa hata 50 kwa siku hizi tatu tutakazokuwepo, na labda tukavuka lengo katika mikoa iliyobaki ya Iringa na Mbeya ambayo ndio ya mwisho katika msimu huu wa pili”, alisema Dk Shaaban.
Kwa upande wake Afisa uhusiano wa Taasisi ya GSM ambayo kwa mwaka huu imewekeza zaidi kusaidia sekta ya Afya na Elimu, Khalphan Kiwamba amesema wanafarijika kuona wagonjwa wanakwenda kutibiwa kama walivyodhamiria, maana ndio lengo haswa, kusaidia kupunguza vifo vya watoto ambao wanasadikika kuzaliwa 4000, kwa mwaka lakini kati yao, ni asilimia 25 tu hurudi hospitalini kwa matibabu huku asilimia 75 wakishindwa kutokana na sababu za kiuchumi.

0 maoni:

Chapisha Maoni

Serikali yawafuta machozi wakazi wa Magomeni



Rais Dkt John Magufuli amezirudisha nyumba zote zilizohamishwa kutoka shirika la nyumba NHC kwenda ofisi ya Rais tawala za mikoa na serikali za mitaa TAMISEMI katika mikoa 20.
Akitoa malalamiko yaliyotolewa June 22 mwaka huu na wakazi 644 wa Magomeni Kota, Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi, William Lukuvi alisema, “Rais Magufuli ameagiza kuwa mkataba wa kujengea nyumba wakazi hao ambao Manispaa ya Kinondoni umeshindwa kutekeleza na kwa sasa mkataba huo utatekelezwa na serikali kupitia wizara yake.
Amesema wazee wote wanaoishi katika nyumba hizo zilizohamishwa kutoka shirika la nyumba NHC kwenda TAMISEMI kuwa wasihamishwe hadi utaratibu mpya utakapotolewa na serikali na kuwataka wazee hao kuendelea kulipa kodi kama kawaida.
“Kwahiyo mheshimiwa Rais amefanya uamuzi mwingine kwamba nyumba zote zilizohamishwa mwanzo mwaka 1990 za National Housing kuja TAMISEMI sasa zirudi serikali kuu. Kwahiyo nyumba kama Magomeni na zote zilizopo mikoa 20 yote Tanzania zimehamishwa sasa zitasimamiwa na serikali kuu, ardhi na nyumba zake,” alisema Lukuvi.
Baadhi ya wakazi wa Magomeni wameishukuru serikali kwa uamuzi huo wakiiomba kulishughulikia suala hilo kwa haraka kwani manispaa ya Kinondoni imewazungusha tangu mwaka 2011 nyumba zao zilipovunjwa katika eneo hilo.
Waliongeza kwa kusema lile eneo walilotuvunjia sasa hivi wanapaki magari, wa mwisho alimalizia kwa kusema, “tunaomba serikali itusaidie isionyeshe ubabaishaji kama uliofanyika pale manispaa.”
BY: EMMY MWAIPOPO

0 maoni:

Chapisha Maoni

Jux kayaongea ya moyoni kuhusu EX wake Jack Cliff

December 2013 zilitoka stori kwamba Mtanzania Jackie Cliff ambae ni mrembo aliekuwa na uhusiano na msanii wa Bongo Fleva Jux  amekamatwa na dawa za kulevya huko China.
Sasa najua ni muda mrefu sana mpaka Jux kuingia kwenye headlines zingine za kuwa na uhusiano na Vanessa Mdee lakini hapa ameipa heshima Ayo TV na millardayo.com kuhusu kuzungumza machache ya EX wake Jack Cliff.
‘Kiukweli nipo kwenye maisha mengine mahusiano mengine uwa najaribu kuuliza kwa watu wake wa karibu ebhana vipi umeongea na fulani hivyo yaani, nisiongee uongo imepita muda kidogo sijapata kuwasiliana nae kwahiyo watu ambao ninakutana nao wananiambia yuko sawa na anaendelea vizuri’– Jux

0 maoni:

Chapisha Maoni

Picha za Jezi mpya za Arsenal,staa wa kwanza wa Hollywood aliyeivaa,

Hizi ndio jezi mpya za Arsenal zitakazovaliwa zaidi kwenye msimu huu wa BPL nchini Uingereza kwenye mechi za ugenini, jezi hizi zilitambulisha mjini Las Angeles.
Kwenye kutambulisha hizi jezi mpya staa wa filamu kutoka Marekani Jamie Foxx alikuwepo.
Club legend Freddie Ljungberg aliyeacha soka mwaka 2007 na sasa ni kocha wa timu ya Arsenal ya vijana wenye umri chini ya miaka 16 alikuwepo. Jezi hizi zitatumika kwneye msimu wa 2016>>2017.

0 maoni:

Chapisha Maoni